Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
MWILI wa aliyekuwa kiongozi wa upinzani wa Jamuhuri ya watu wa Kongo Etienne Tshisekedi ambaye pia ni Rais wa sasa wa nchi hiyo Felix Tshisekedi umewasili nchini humo leo baada ya kuhifadhiwa nchini Ubelgiji baada ya kufikwa na umauti takribani miaka miwili iliyopita.

Wanafamilia wameeleza kuwa kuwa mwili utawasili kutoka Ubelgiji na kuzikwa kwa heshima nchini humo, Etienne alifariki mwaka 2017 Februari huko Brussels huko Ubelgiji akiwa na miaka 84 na mwili wake kuhifadhiwa huko kwa wasiwasi wa kiusalama.

Imeelezwa kuwa mwili wake utazikwa kwa heshima na maandalizi ya mazishi hayo yamekamilika.

Mazishi hayo yatahudhuriwa na marais mbalimbali huku ikielezwa kuwa atazikwa kama shujaa.

Mwanaye wa kiume Felix Tshisekedi aliapishwa kuwa Rais wa nchi hiyi Januari 24 mwaka huu akifuata nyayo za baba yake ambaye alikuwa mkosoaji  mkubwa dhidi ya dikteta Mobutu Sese Seko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 30, 2019

    Uyo felix ambaye pia ni rais wa sasa? na alisha kufa kabla ya kuwa rais����

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...