Na Humphrey
Sahao, Globu ya Jamii.
Mkuu wa mkoa
wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wakazi wa jiji hilo kuacha kutumia
muda mwingi kuongelea mambo ya watu na kutumia muda huo kufanya kazi na
kuzalisha hili kusaidia uchumi wa taifa hili.
Makonda
amesema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa mbagala wakati wa kuhitimisha
Tamasha la Shika Ndinga linaloendeshwa na kituo cha Radio cha EFM cha Jijini
Dar es Salaam.
“kumekuwa na
tabia ya ajabu sana katika mkoa huu watu wanatumia muda mwingi kuzungumza
mbambo ya watu na kuacha kufanya kazi hali inayofanya wageni kutoka mikoa
mingine kufika hapa na kufanya maendeleo na kuchukua fursa zilizopo huku
wenyeji wakibaki kulalamika vibarazani”amesema Rc Makonda.
Ametaja kuwa
Jiji la Dar es Dasalaam ndio jiji linaloongoza kwa fursa nyingi za kujipatia
kipato lakini wazaliwa wa hapa wamebaki kuwa maskini kutokana na kufanya mambo
yao kwa mazoea hivyo kuwataka sasa waamke na kutumia fursa zilizopo kujiletea
maendeleo.
Aidha
makonda alitumia fursa ya kusanyiko hilo kuwakumbusha Vijana kujitokeza kwa
wingi katika kujiandikisha katika Daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi
wa serikali za Mitaa.
Pia
amewataka Vijana kutumia muda huu kujitokeza kuchukua fomu na kugombea nafasi
mbalimbali za uongozi.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na Wakazi wa Mbagala Zakhem wakati wa kuhitimisha fainali za shika ndinga jijini Dar es Salaam zinazoa andaliwa na kituo cha Radio ya Efm.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akikabidhi zawadi ya gari kwa mshindi wa kike ambaye ametokea mkoa wa Mtwara.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikabidhi zawadi ya gari kwa Mshindi wa kiume ambaye ametokea mkoa wa Dodoma.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambo sasa akieleza hali ya Usalama
Washiriki wakiwa katika hatua ya kufungua Toelet Pepa
Washiriki wakiwa katikahatua ya kukimbia na kitenesi
Majaji wa shindano la shika ndinga wakiwa makini kusimamia mchuano katika Viwanja vya Zakhem
Washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari
Washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari
Wageni wa Meza wa Meza kuu wakisuhudia washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari
Eneo la uwanja wa mshindano ya shika ndinga linavyoonekana kwa juu
--
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...