Na Humphrey Sahao, Globu ya Jamii.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wakazi wa jiji hilo kuacha kutumia muda mwingi kuongelea mambo ya watu na kutumia muda huo kufanya kazi na kuzalisha hili kusaidia uchumi wa taifa hili.

Makonda amesema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa mbagala wakati wa kuhitimisha Tamasha la Shika Ndinga linaloendeshwa na kituo cha Radio cha EFM cha Jijini Dar es Salaam.

“kumekuwa na tabia ya ajabu sana katika mkoa huu watu wanatumia muda mwingi kuzungumza mbambo ya watu na kuacha kufanya kazi hali inayofanya wageni kutoka mikoa mingine kufika hapa na kufanya maendeleo na kuchukua fursa zilizopo huku wenyeji wakibaki kulalamika vibarazani”amesema Rc Makonda.

Ametaja kuwa Jiji la Dar es Dasalaam ndio jiji linaloongoza kwa fursa nyingi za kujipatia kipato lakini wazaliwa wa hapa wamebaki kuwa maskini kutokana na kufanya mambo yao kwa mazoea hivyo kuwataka sasa waamke na kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo.

Aidha makonda alitumia fursa ya kusanyiko hilo kuwakumbusha Vijana kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha katika Daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za Mitaa.

Pia amewataka Vijana kutumia muda huu kujitokeza kuchukua fomu na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na Wakazi wa Mbagala Zakhem wakati wa kuhitimisha fainali za shika ndinga jijini Dar es Salaam zinazoa andaliwa na kituo cha Radio  ya Efm.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akikabidhi zawadi ya gari kwa mshindi wa kike ambaye ametokea mkoa wa Mtwara.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikabidhi zawadi ya gari kwa Mshindi wa kiume ambaye ametokea mkoa wa Dodoma.
  Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambo sasa akieleza hali ya Usalama
 Washiriki wakiwa katika hatua ya kufungua Toelet Pepa 
 Washiriki wakiwa katikahatua ya kukimbia na kitenesi  
 Majaji wa shindano la shika ndinga wakiwa makini kusimamia mchuano katika Viwanja vya Zakhem 
 Washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari 
 Washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari
 Wageni wa Meza wa Meza kuu wakisuhudia washiriki wakiwa hatua ya fainali hili waweze kuchukua gari
 Eneo la uwanja wa mshindano ya shika ndinga linavyoonekana kwa juu 

--

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...