Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ( kulia), akisalimiana na Meneja wa Benki ya Biashara ya DCB Tawi la Dodoma, joseph Njile wakati Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Godfrey Ndalahwa (katikati), akimtembelea waziri mkuu, ofisini kwake, bungeni Dodoma.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ( kulia), akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (katikati) pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo, walipomtegembelea waziri mkuu, ofisini kwake, bungeni Dodoma.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ( katikati), akipiga picha na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (wa pili kushoto) pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo, walipomtembelea waziri mkuu, ofisini kwake, bungeni Dodoma jana. Kutoka kushoto ni, Rahma Ngassa, Joseph Njile na Nuru Ashraf (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameupongeza uongozi benki ya DCB kwa kufanikiwa kubadili muundo kutoka benki ya jamii na kuwa ya biashara kwani kuna benki nyingi ambazo zimeshindwa kujiendesha.

Akizungumza na uongozi wa benki hiyo, alipokutana na uongozi wa benki hiyo ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema benki nyingi za jamii zimekufa baada ya kushidwa kujiendesha lakini kwa benki ya DCB wameweza kumudu kujiendesha hadi kufikia kuwa benki ya biashara.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa benki hiyo uimarishe kitengo cha elimu kwa umma ili jamii ifahamu huduma wanazozitoa."Nendeni kwa wananchi mkawape elimu kuhusu umuhimu wa kufungua akaunti na pia rahisisheni mazingira ya kutolea huduma kwa wateja."

Pia Waziri Mkuu ameitaka benki hiyo isogeze huduma kwa wananchi hususan maeneo ya pembezoni ambayo bado hayajafikiwa. Amesema ni muhimu wananchi wakasogezewa huduma za kibenki ili waweze kuhakikishiwa usalama wao pamoja na fedha zao.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Godfrey Ndalahwa amesema tangu benki hiyo ianzishwe imefanikiwa kukuza amana za wateja kutoka Sh. bilioni mbili mwaka 2002 hadi Sh. bilioni 75 Desemba mwaka 2018. Pia mikopo imeongezeka kutoka Sh. bilioni moja mwaka 2002 na kufikia Sh. bilioni 90, Desemba 2018, faida ikiwa ni Sh. bilioni 17.7 baada ya kodi.”

Mkurugenzi huyo alisema katika kipindi cha miaka 16 ya utendaji wake, benki hiyo imeshatoa gawio la zaidi ya Sh. bilioni 11 kwa wanachama wake huku akitumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli kwa kuboresha maendeleo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...