Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Liberatus Sabas, mapema leo amefunga mafunzo katika Eneo la mafunzo liliopo Kilelepori wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kwa askari wanaotunza Silaha na Vielelezo vilivyopo ndani ya vituo vya polisi katika sehemu mbalimbali, katika
hatua hiyo amewataka Askari kutenda kazi kwa kuzingatia Maadili na
Weledi ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi hii itasaidia
kuepuka kupotea kwa vielelezo hivyo. 

Aidha katika hatua hiyo amewaonya Askari Polisi wanaoomba na kupokea rushwa kutoka sehemu mbalimbali hasa kwa wafanyabiashara na watu wengine wenye nia njema ya kuhakikisha Uchumi wa Nchi unapanda na kufikia uchumi wa kati, Jeshi la Polisi halitamuonea muhali askari yoyote bali atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi kisha kufikishwa mahakamani kwa kufanya hivyo Jeshi la Polisi litakuwa limemuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Joseph Magufuli katika kuhakikisha nchi yetu inafikia uchumi wa kati. 

Amemalizia kwa kuwataka wale wote wanaotaka kuvunja amani au kuchezea amani ya nchi yetu watachukuliwa hatua kali ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na amani kama ilivyo na inavyofahamika kuwa Tanzania ni kisiwa cha amani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...