Ofisi ya Makamu wa Rais katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma leo imefanya usafi katika eneo la Makulu jijini Dodoma kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji, NEMC, Wadau mbali mbali wa mazingira pamoja na Wananchi wa Makulu.
Wananchi na Wadau wa Mazingira wakishiriki zoezi la usafi katika eneo la Makulu, Dodoma ambapo taka za mifuko ya plastiki zilipewa kipaumbele, zoezi hili liliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wakazi wa Makulu jijini Dodoma wakiwa na vifaa vyao vya usafi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (hayupo pichani) kabla ya kuanza kwa zoezi la usafi lililoratibiwa na Ofisi yake ikiwa Sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wananchi na Wadau wa Mazingira wakishiriki zoezi la usafi katika eneo la Makulu, Dodoma ambapo taka za mifuko ya plastiki zilipewa kipaumbele, zoezi hili liliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, Wadau wa mazingira na Wananchi mara baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Makulu Dodoma, zoezi hilo liliratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, Wadau wa mazingira na Wananchi mara baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Makulu Dodoma, zoezi hilo liliratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (mwenye kofia) akiongoza watumishi wa ofisi yake pamoja na wananchi wa Makulu, Dodoma kufanya usafi ikiwa sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (mwenye kofia) akiongoza watumishi wa ofisi yake pamoja na wananchi wa Makulu, Dodoma kufanya usafi ikiwa sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...