*Ndugu Wanafamilia na Watanzania Wote Waishio UK *
Uongozi
wa Jumuiya ya Watanzania nchini Uingereza TZUK DIASPORA kwa masikitiko
makubwa inawatangazia taarifa ya msiba wa Mke wa mwanajumuiya mwenzetu
Abdulkadir Rashid , Bi Rachel Maona kilichotokea leo asubuhi tarehe
08/06/2019 Keech Hospices - Luton nchini Uingereza.
Marehemu
Bi. Rachel Maona ambaye alikuwa akifanya kazi Luton and Dunstable
Hospital nchini Uingereza alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Kansa na
ameacha watoto watatu na mume.
Taratibu
za msiba na kusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Tanzania kwa
mazishi zinaendelea kufanywa kwa kushirikiana na East Africa Muslim
Community na Luton Tanzanian Community , Kwa kushirikiana na watanzania
wanaoishi UK.
Wanajumuiya,
Watanzania, Ndugu, Jamaa, na marafiki Uongozi kwa niaba ya familia ya
tunawaomba ushirikiano wenu na faraja kwa familia.
UONGOZI
JUMUIYA YA WATANZANIA WAISHIO UK (TZUK DIASPORA



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...