Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro amekagua mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi hilo zinazojengwa katika eneo la Magugu mkoani Geita, mradi unaotekelezwa kutokana na fedha iliyotolewa na Mhe. Rais John Magufuli. 

Katika ukaguzi huo IGP Sirro mesema kuwa, hadi sasa maendeleo ya ujenzi wa nyumba hizo umefikia katika hatua nzuri na kwamba amewaomba wadau wengine welevu kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuendelea kuboresha makazi ya askari jambo ambalo litasaidia kuwajengea morali wakati wanapotimiza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...