Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda, leo Julai 29 amezindua kampeni ya tano ya usafi yenye lengo la kuendeleza kufanya usafi wa jiji Dar es Salaam ikiwa ni hatua za maandalizi ya kupokea ugeni wa viongozi wa Umoja wa Nchi zilizo Kusini Mwa Afrika (SADC).

Akizungumza na waandishi wa Habari Julai 29/2019 katika uzinduzi Kampeni ya Usafi katika Uwanja wa Ndege Terminal I,Makonda amesema lengo kubwa ni kuweka Jiji Safi huku akizitaka Taasisi zote za Serikali kuhakikisha kwamba zinakuwa na watu wao wa usafi katika maeneo yao ya kazi.

Makonda amesema pamoja na kuweka Jiji la Dar es Salaam kuwa safi ni kuonyesha ubora wa wananchi wa jiji hilo na mikoa mingine ifanye hivyo na wakija wajifunze vitu vingine ikiwemo usafi kutokana na kuwepo Marais 16 katika mkutano wa SADC. 

Amesema kuwa Mkoa wa Dar Es Salaam unachangamoto ya usafi hivyo ni vyema wakajenga utamaduni wa kufanya usafi Mara kwa Mara.

"Nataka kuwaambia tu kwamba nimemsikia Mratibu wa kila Taasisi ya Serikali katika mkoa wangu iwe na watu wa usafi" Amesema RC Makonda.Amesema ugeni wa SADC ni heshima kwa Rais Dkt John Magufuli na Mkoa wa Dar Es Salaam kwa ujumla hivyo lazima Jiji liwe safi wakati wa kuwapokea wageni pia usafi huo uwe endelevu.

Katika hotuba yake Makonda amewataka wakazi wa Dar Es Salaam, kuzingatia usafi na kupiga marufuku mtu yoyote kufika mjini kama hajafanya usafi wa mwili wake ikiwemo kuoga, kufua na kupiga pasi nguo zake.

“Tabia ya kuja mjini hujafua, hujaoga usitutie aibu kama umezoea kuja mjini hujaoga wala kufua nguo baki nyumbani walau huu mwezi wa nane uishe, tunataka sio usafi tu wa mazingira, usafi pia wa wananchi wetu, watu wamejaa chawa tu hapa”. Amesema.

“Ule utaratibu wetu wa Lugalo tunauanza rasmi leo haiwezekani wawe na nidhamu kwenye kile kipande cha kukaribia mita 200, 300 kwahiyo ule utaratibu wa mtu kwenye gari kutupa taka hovyo mshusheni akikataa chukueni namba yake ya gari tutamkamata ili aje apige deki” Amesema Makonda.

Pia amesema ifikapo Agosti 5 Jiji la Dar Es salaam liwe safi kwa ajili ya mapokezi ya wageni na amewataka Maafisa Mazingira kuhakikisha miti yote inayopandwa inaota kwani Serikali imekuwa ikitenga bajeti kubwa na pesa hizo hazioneshi matunda na Mazingira chanya kama inavyokusudiwa.

Makonda amewataka Vijana wa usafishaji kuhakikisha kwamba Dereva wa gari akitupa taka taka hovyo apigishwe deki kwa kupewa kipande cha bara bara badala ya kuwapiga faini za pesa na watendaji wa mitaa husika kuhakikisha maeneo yao yanakuwa safi la sivyo watapoteza ajira zao.

Katika hatua nyingine amewataka Wananchi na Tanzania kwa ujumla wajitokeze kwa wingi katika uzinduzi wa Uwanja mpya wa ndege wa Kisasa wa Mwalimu Nyerere Terminal 3 wenye uwezo wa kubeba Abiria Milioni 6 utakaotarajiwa kuzinduliwa na Rais Dkt John Magufuli Agosti 4/2019 asubuhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...