Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), inatoa huduma mbalimbali ikiwamo vyeti vya kuzaliwa katika Maonyesho 43 ya biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.

Meneja Masoko na Mawasiliano wa RITA, Josephat Kimaro amesema mbali na kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa pia wakala utatoa ushauri wa kisheria bure kuhusu masuala ya kuandika wosia na mirathi.

“Pia tutapokea maoni, maswali, ushauri na mapendekezo kuhusu huduma za Wakala,” amesema.Kimaro amesema RITA imekuwa ikishiriki maonesho hayo kila mwaka ambapo amewaomba wananchi wakifika sabasaba watahudumiwa kwa bora kwa wakati. 
Baadhi ya wananchi wakipata huduma ya vyeti vya kuzaliwa katika banda la Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) leo katika maonesho ya 43 ya Kimataifa Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa RITA, Josephat Kimaro (kushoto) akizungumza kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo ikiwamo vyeti vya kuzaliwa katika maonesho ya 43 ya Kimataifa Sabasaba jijini Dar es Salaam. Watumishi wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), wakiwaelekeza wananchi namna ya kujaza fom za cheti cha kuzaliwa leo katika maonesho ya 43 ya Kimataifa Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...