Baadhi ya madarasa yaliyofanyiwa ukarabati na Taasisi za Chemchem Association.
Kikao cha vikoba wananchi wa vilima vitatu kikiendekea
Madawati yametolewa na Kampuni ya Taasisi za Chemchem Association shule msingi Vilima vitatu.
Baadhi ya madarasa yaliyofanyiwa ukarabati na Taasisi za Chemchem Association ambapo kwa jumla yake yapo saba.Hayo madawati yametolewa shule msingi Vilima vitatu, na hiyo ndio shule iliyokarabatiwa na hapo kikao cha vikoba wananchi wa vilima vitatu

Na Vero Ignatus,Arusha

Zaidi ya sh 100 milioni imepangwa kuchangia miradi ya Maendeleo katika eneo la Jumuiya ya hifadhi ya jamii ya Wanyamapori( JUHIBU kutoka kwa Taasisi za Chemchem Association.

Taasisi hiyo ya JUHIBU, ilianzishwa mwaka 2003 ambapi inaundwa na vijiji vyaangawe,Mwada,Ngoley,Vilimavitatu,Minjingu,Kakoi,Olasiti,Manyara,Magala, na Maweni na ina ukubwa wa 283.

Walter Palangyo ni Afisa Maendeleo ya jamii ya Taasisi ya Chemchem association, amesema taasisi inachangia miradi hiyo kama sehemu ya wajibu wake kuchagia shughuli za Maendeleo ya jamii(SCR) mbali ya kodi na tozo nyingine zinazolipwa na Chemchem iliyowekeza shughuli za Utalii katika hifadhi hiyo.

Amesema taasisi hiyo, imekamilisha ukarabati wa majengo ya shule ya msingi vilima vitatu,ofisi mbili za walimu na sasa ipo kwenye mradi wa ujenzi wa vyoo ."katika shule hii, tumetumia kiasi cha sh 50 milioni, ili kuhakikisha wanafunzi katika shule hii wanapata elimu bora katika mazingira mazuri kwani tayari tumewapatia madawati 100 kwa ili kumaliza tatizo katika shule hii"alisema

Amesema taasisi hiyo pia imetoa kiasi cha sh 5 milioni ili kusaidia Vikoba katika baadhi ya vijiji katika eneo hilo, ikiwepo vikundi vya jamii ya wabarbeig ili kuweza kuwa na miradi ya maendeleo."Kuna kikundi cha Wicheda na Datoga vya jamii ya Kibarbeig ambavyo tumepatia kiasi cha sh 2.5 milioni ili kukuza mitaji yao"alisema

Alisema katika jamii hiyo, pia kumeanzishwa mradi wa maboma ya asili ambayo watalii wataweza kuwatembelea ."Mwaka huu pia tunaendelea na mradi wa kusomesha watoto katika jamii hii, katika chuo cha wanyamapori cha Mweka na chuo cha Ufundi (VETA) naa wengine tumewalipia ada za shule ya sekondari "alisema

Amesema pia kuna miradi ya maji, michezo na afya katika vijiji hivyo, hasa kutokana na fedha ambazo zinatokana na la ya utalii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...