Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira jijini Mwanza (MWAUWASA) imetoa ufafanuzi kuhusu mabadiliko mapya ya ankra za maji huku ikitumia fursa hiyo kuwaelekeza wafanyabiashara wa maji kwamba bei elekezi kwa ndoo moja ya maji yenye ujazo wa lita 20 ni shilingi 50 tu.

Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga alitoa ufafanuzi huo Agosti 09, 2019 kwenye ziara ya waandishi wa habari mkoani Mwanza kutembelea miradi mbalimbali ya maji inayosimamiwa na mamlaka hiyo ili kujifunza utendaji kazi wake.
Na George Binagi-GB Pazzo, Mwanza
 Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA, Mhandisi Antony Sanga akitoa ufafanuzi kwa wanahabari (hawako pichani)  kuhusu miradi ya maji inayosimamiwa na mamlaka hiyo pamoja na ongezeko la bei mpya ya maji.
 Wanahabari walitembelea eneo hili la mradi wa maji Capripoint jijini Mwanza kujifunza maji yanavyosafishwa na kutibiwa kabla ya kumfikia mtumiaji.
 Mradi wa maji MWAUWASA Capripoint jijini Mwanza.
Wanahabari pia walitembelea mradi mpya wa maji Nyahiti wilayani Misungwi na kushuhudia kwa mara ya kwanza mashine za kusukuma maji zikiwashwa kwenye mradi huo.
 Tenki kubwa la kusambazia maji katika mji wa Misingwi kutoka chanzo cha maji Nyahiti.
 Ziara hii iliratibiwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC) ikilenga pia kuimarisha mahusiano na MWAUWASA.
Tazama Video hapa chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...