Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kutoa burudani kwa wageni mbalimbali walioalikwa katika chakula cha jioni. Hafla iliyoandaliwa kwa ajili ya ukaribisho wa wageni wa Mkutano wa SADC hususan wa wale wa Wizara ya Viawanda na Biashara.
Mgeni Rasmi katika hafla hio alikua Mheshimiwa Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikitoa burudani kwa wageni katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City. Ngoma hii inaitwa Druming Ensemble ambayo ni mchanganyo wa upigaji wa ngoma mbalimbali za kitanzania kwa kundi.

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Balozi Amina Salum Ali (aliyevaa miwani) alikua mmoja wa wageni waliohudhururia hafla hio na kuonyesha kufurahia uchezaji wa ngoma uliyofanywa na kikundi cha ngoma kutoka TaSUBa.
Waimbaji wa Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) wakiimba kwa kupokezana katika ngoma ya Nsimba ambayo inabebwa na uimbaji wa majibishano. 
Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikicheza kwa madaha ngoma ya Nsimba ambayo huchezwa kwa kutumia ala ya vyungu ambayo asili yake huchezwa na wanawake wa kabila la kifipa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...