JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA (KUSHOTO) AKIMKABIDHI MKUU WA WILAYA YA MUFINDI MHE. JAMHURI WILLIAM KITABU CHA MPANGO WA MIAKA MITANO WA UJENZI WA MAJENGO YA MAHAKAMA YA TANZANIA ALIPOMTEMBELEA OFISINI KWAKE AKIWA KATIKA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA.


JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WATUMISHI WA MAHAKAMA YA WILAYA YA MUFINDI BAADA YA KUZUNGUMZA NAO ALIPOTEMBELEA MAHAKAMA YA WILAYA YA MUFINDI KUKAGUA SHUGHULI ZA MAHAKAMA AKIWA KATIKA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA

MKUU WA WILAYA YA MUFINDI MHE. JAMHURI WILLIAM AKIMUELEZEA JAMBO JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA WAKATI JAJI MKUU ALIPOENDA KUKAGUA KIWANJA CHA UJENZI WA JENGO LA MAHAKAMA YA MWANZO MJINI MAFINGA AKIWA KATIKA ZIARA YA KIKAZI MKOANI IRINGA.
********************
Lydia Churi-Mahakama Iringa
Mahakimu wametakiwa kusimamia uendeshaji wa mashauri na kuzuia maahirisho ya mara kwa mara ya kesi bila ya sababu za msingi kwa lengo la kuhakikisha kesizinamalizika kwa wakati Mahakamani.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema hayo wakati wakikao cha majumuisho mara baada ya kumaliza ziara ya kikazi ya siku tano katikamikoa ya Iringa na Njombe aliyoifanya kwa lengo la kukagua shughuli zaMahakama pamoja na kubainisha kwa wadau changamoto zilizoibuliwa wakati wakikao cha Mahakama ya Rufani kilichomalizika leo mjini Iringa.
Jaji Mkuu amewata Mahakimu kutokubali kuahirisha mashauri kwa muda mrefukwa ajili ya kuandaa maamuzi madogo yanayotokana na pingamizi ambazo nyingihutumiwa vibaya kwa lengo la kuchelewesha mashauri.
“Maafisa wote wa Mahakama ni jukumu lenu pia kuzipa nguvu za kimahakamavifungu vya sheria zinazolinda haki ya Mwananchi aliye mahabusu kwakuhakikisha hakuna mwananchi atashikiliwa bila kufikishwa mahakamani ndani yasiku zilizowekwa na sheria”, alisema.
Alitoa rai kwa Mahakimu kutokuwa wepesi kukubali hoja za waendesha mashitakaza kusema kuwa upelelezi bado unaendelea bila ya kufafanua ni kitu gani katikaupelelezi bado kinatafutwa na ni kwa muda gani.
“Ni umakini wa Mahakama ndiyo utahakikisha kuwa shughuli za upelelezi
haziwanyimi wananchi haki yao ya kikatiba ya kutochelewesha haki yao ya
kusikilizwa kesi dhidi yao bila sababu za kimsingi,” alisisitiza Jaji Mkuu.
Akizungumzia dhamana, Jaji Mkuu amesema ni wajibu wa Mahakama kutoa
dhamana kwa makosa yenye dhamana kwa kuwa Mahakama ni msimamizi wahaki ya kila mtu kuwa huru na kuishi kama mtu huru.
Alivitaja vigezo vya kutumiwa katika kutoa dhamana kuwa ni pamoja na
vitambulisho vya Taifa, na vitambulisho vinavyokubalika. Aliongeza kuwa
Mahakama pia ziwaruhusu washtakiwa kujidhamini wenyewe pale Hakimu
anapojiridhisha na utambulisho wao kuwa watahudhuria mahakamani.
“Mashauri ambayo washtakiwa wamekosa dhamana yasikilizwe mfululizo, kwayale makosa yasiyo na dhamana na yako ndani ya mamlaka ya Mahakama,matumizi ya sheria yatumike ili kuyaondosha”, alisema.
Katika kupunguza msongamano magerezani, Jaji Mkuu amesema Maafisa waMahakama hawana budi kutumia adhabu mbadala kwa makosa madogo madogokwa kuzingatia sheria zilizopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...