Wachezaji wa Timu ya Simba wakipanda gari kuelekea Hotelimara baada ya kuwasili Bukoba.
Kocha wa Timu ya Simba Patrick Aussem.

Anaadika Abdullatif Yunus - Michuzi TV.
WEKUNDU wa msimbazi Timu ya Simba Sports Club wamewasili salama Mjini Bukoba Majira ya Saa  tatu kwa usafiri wa anga, tayari kuziwinda pointi tatu muhimu dhidi ya wenyeji wao Kagera sugar.

Katika hali ya isiyo ya kawaida Timu hii ya Simba imewasili kimya kimya Mjini Bukoba tofauti na miaka iliyopita, ambapo hali ya mapokezi imeonekana kuwa hafifu bila kushuhudia zile mbwembwe, shamra shamra za mashabiki licha ya baadhi ya mashabiki ndaki ndaki wa boda boda kujitokeza kuipokea Timu na kisha kuisindikiza hadi Hotelini.

Akizungumza Mara baada ya kutua katika kiwanja cha Ndege cha Bukoba, Kocha wa Timu ya Simba Patrick Aussems amesema "..Timu imekuwa kambini takribani siku tatu, na tayari imewasili salama Bukoba, tutakuwa na mazoezi mepesi mchana tayari kwa mchezo wa kesho, ingawa Kagera Sugar imekuwa ikimpiga Simba, lakini Mara hii tumejiandaa.." Amesema Aussems

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...