Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, ( CGF) Thobias Andengenye (aliyeshika bendera) akiongoza msafara wa askari 11 wa jeshi hilo kupanda mlima Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye (kulia) akiongoza msafara wa askari 11 wa jeshi hilo kupanda mlima Kilimanjaro.

**************************
KAMISHNA Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CGF) Thobias Andengenye amewaongoza maofisa 11 wa jeshi hilo kupanda mlima Kilimanjaro kwa kuitaka jamii kuwa wazalendo kwa kupenda utalii wa ndani na kutembelea hifadhi za Taifa. 

Akizungumza jana kamishna Jenerali Andengenye alisema watanzania wanapaswa kupenda vivutio vya utalii wa ndani. 

Alisema askari watapanda mlima Kilimanjaro kujionea ufahari uliopo ili kukuza uchumi wa nchi wakiwawakilisha askari wa zimamoto wengine hapa nchini.
Alisema wenyewe wanahusika na dharura zote za uokoaji isipokuwa za jinai ndiyo sababu wakaonelea wapande juu ya Afrika kupitia mlima Kilimanjaro ambao ni mrefu kwenye bara hilo. 

“Sisi tunapaswa tutumie karama tuliyopewa na Mungu kwa kutembelea na kujionea ili kukuza uchumi wetu kwa watanzania wenyewe kuchangia pindi tukitembelea hifadhi zetu,” alisema Andengenye. 

Mkaguzi msaidizi wa jeshi la zimamoto na uokoaji, Bilhah Chaila akizungumza wakati wakijiandaa kupanda mlima Kilimanjaro aliwahamasisha wanawake wa ndani na nje ya nchi kushiriki kwa wingi kwenye vivutio vya utalii. 

Chaila alisema kuwa wanawake wanauwezo mkubwa kama wanawake hivyo wanapaswa kushiriki kuchangia pato la Taifa kwa kutembelea hifadhi za Taifa zilizopo sehemu mbalimbali hapa nchini. 

Kamishna Jenerali Andengenye na maofisa hao 11 wanatarajia kupanda mlima Kilimanjaro na kurejea ijumaa ijayo Octoba 4 mwaka huu. Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu zaidi barani Afrika una urefu wa karibia mita 6,000 sawa na zaidi ya futi 20,000.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...