Na Leandra Gabriel, Michuzi Tv
KWA mujibu  ya mtandao wa Worldometers unaofuatilia matukio yanayotokea duniani kwa kila sekunde, leo Oktoba 18 idadi ya watu nchini India imefikia 1,370,455,147 kwa mujibu wa data za umoja wa Mataifa.
Kwa mujibu wa wa data za mwaka 2018, China nchi inayoongoza kwa kuwa na watu wengi zaidi duniani iliizidi India kwa zaidi ya watu milioni 41 na kufanya  nchi hizo mbili kubeba asilimia 36.28 ya idadi ya watu 7,632,819,325 duniani kote kwa mwaka 2018.
Licha ya India kuwa na watu wengi zaidi bado imeendelea kutunza na kuhifadhi Miji na maeneo mbalimbali ambayo hutembelewa na watalii, kwa mujibu wa jarida la Culture Trip la India Miji maarufu na yenye kuvutia zaidi nchini humo ni pamoja na ;
Jaipur
Mji huu hujulikana zaidi kama “Pink City”na hiyo ni kutokana na majengo yake kupakwa rangi ya Pinki mwaka 1976 wakati wakimkaribisha Malkia Victoria na mwana mfalme wa Wales.
Pembe tatu ya dhahabu na mahekalu huwavutia maelfu ya Wahindi na watalii kutoka nje ya nchi kila mwaka.
Veranasi
Umaarufu wa Mji huu ni kubeba historia ya kiimani huko Kaskazini mwa India, historia yake ilianza karne ya 11 baada ya Kristo na inaelezwa kuwa hii ni sehemu kongwe zaidi duniani. Mji huu umebeba mahekalu mbalimbali, makuhani, wajasiriamali na makazi ya watu.
Udaipur
Mji huu ni maarufu zaidi kwa maziwa (Lakes,) ngome, makanisa pamoja na majumba ya kifalme, unapatikana Rajasthan na hupendelewa zaidi na wapendanao kutokana na bustani nzuri za kuvutia zipatikanazo pia filamu nyingi zimechezwa Udaipur ikiwemo ya James Bond- Octopussy (1983) pia sherehe mbalimbali hufanyika katika Mji huo.
Bangalore
Umaarufu wa Mji huu hutokana na uwepo wa viwanda vingi vya teknolojia ya kompyuta, na hujulikana zaidi kama ‘Silicon Valley’pia Mji wenye misitu ya kijani inayowatia wengi na umeendelea katika masuala ya taaluma.
Delhi
Ni Mji mkuu wa nchi na Serikali, licha ya kufahamika hivyo Delhi imebeba tamaduni na shughuli zake ikiwemo michoro na sanaa mbalimbali, sehemu nyingi za kupata chakula kwa wageni hupatikana Delhi na hiyo ni pamoja na kuwepo kwa makanisa, misikiti, na ngome maarufu zaidi zikiwemo Red Fort, Jama Masjid na ngome ya Baha’i Lotus.
Chennai
Ni Mji wa kiutamaduni, michoro ya utamaduni na huwavutia wageni wengi zaidi na ni maarufu zaidi kwa watalii.
Mysore
Unapatikana Kusini mwa India, na ni moja kati Mji uliopangwa vizuri nchini humo,  Mji wa pili kwa usafi India huku ukiwa mji wa tamaduni zaidi huko Karnataka. Pia Mji huu ni maarufu kwa mchezo wa Yoga ( Ashtanga Yoga ilianzia hapa.)
Agra
Mji huu ni sehemu ya maajabu saba ya dunia, umaarufu wa Agra ni kutokana na sehemu mbili za urithi wa shirika Umoja wa mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni  (UNESCO) ya Agra Fort na Fatehpur Sikri.
Kolkata
Ni Mji wa utamaduni ambao watu maarufu wakiwemo waimbaji, waigizaji, waandishi, washindi wa tuzo za Nobel na watayarishaji wa filamu wanaishi. Pia Mji huo una hazina ya vyuo vya utalii na bustani nyingi za maua.
Mumbai
Mji huu ulianza mwaka 1911, upo pembezoni mwa bahari na hapo awali ulijulikana kama Bombay, ni kitovu cha uchumi pamoja na vivutio vya utalii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...