Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

MFANYABASHARA, Elizabeth Balali (54) ambaye anadaiwa kuwa msimamizi wa Mirathi za mke wa marehemu Daud Balali, mkazi wa Boko Magengeni jijini Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kujipatia Sh milioni 25 kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha wa fedha.

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa serikali Mwandamizi, Simon Wankyo amedai Mbele ya Hakimu mkazi Mfawidhi, Kelvin Mhina kuwa kati ya Oktoba 19 na Desemba 21, 2017 Dar es Salaam mshtakiwa alijipatia kiasi cha Sh 25 milioni kutoka kwa Dk Roderick Kisenge kwa njia ya ulaghai akijifanya anamuuzia eneo la squre mita 900 ambalo halijapimwa lililopo eneo la Boko Dovya Kinondoni wakati akijua kuwa eneo hilo si lake.

Katika shtaka la pili imedaiwa, siku na mahali hapo hapo mshtakiwa huyo alipokea kiasi hicho cha Sh. Milioni 25 kutoka kwa Dk Kisenge kupitia akaunti yake iliyopo kwenye benki ya CRDB wakati akijua fedha hizo ni zao la kosa tangulizi la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo,Elizabeth hakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikilizwa makosa ya Uhujumu Uchumi na pia shtaka la utakatishaji wa fedha halina dhamana.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika, Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 24, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na mshtakiwa alipelekwa rumande.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...