RAIA wa China, Cheng Guo, anayeshuka kwenye gari, ameiarifu mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa yeye hajaandika barua ya kukiri makosa yake ila ameandika barua ya kulalamikia kucheleweshwa kwa kesi yake na kuomba msamaha.
Katika kesi hiyo, mshtakiwa anakabiliwa na mashitaka ya kukutwa na nyara za serikali ambazo ni meno ya Tembo na kucha za Simba ambapo vyote vina thamani ya zaidi ya sh. Milioni 267. 4.
Mshitakiwa Guo amedai hayo leo Oktoba 4, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi wakati alipoletwa mahakamani hapo kwa hati ya kutolewa gerezani.
"Nimeandika barua nimesema kesi imechukua muda mrefu pia ninaomba msamaha, sijasema nataka kulipa pesa", amedai mshitakiwa Guo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...