Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akieleza jambo kwa Wanakamati ya Maandalizi alipotembelea Uwanja wa Ilulu kukagua maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika Mkuani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea uwanja wa Ilulu kukagua maandalizi ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Andrew Massawe.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na watoto wa halaiki alipowatembea kwa ajili ya kukagua maandalizi yao kuelekea Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Sehemu ya watoto wa halaiki wakifanya mazoezi ya utayarisho kuelekea Kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika Mkoani Lindi Oktoba 14, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipokea mwamvuli kutoka kwa Meneja wa Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania kanda ya Lindi Bw. Zephania Ludigija itakayotumiwa na Watoto wa Halaiki.PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...