Na.Khadija seif, Michuzi TV.

 JAJI Mkuu wa shindano la kusaka vipaji (BSS) Rita paulsen ajibu malalamiko ya kijana Hamisi kutolewa kwenye mashindano hayo.

Usiku wa kuamkia leo Jumanne Novemba 18, 2019 wafuatiliaji wa kipindi cha Bongo Stars Search wamechukizwa na kitendo cha mshiriki wa shindano hilo, Hamisi kutolewa kwenye kinyang’aro hicho.

Madam Rita amesema kuwa kijana huyo, Bado yupo ila kasimamishwa kutokana na ishu za masomo na ataendelea kushiriki.

 “Yupo sana alitakiwa kuondoka ili kumalizia mitihani yake ya kidato cha nne ila yupo kambini,” Ameeleza Madam Rita kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwatuliza watazamaji wa shindano hilo.

Jana Hamisi alishindwa kuingia kwenye Top 20 ya washiriki ambao wameingia kambini na kujikuta akitolewa kwenye mashindano hayo, Huku majaji wakieleza kuwa endapo watazamaji wangependa kumuona Hamisi au washiriki wengine waliotolewa kwenye Top 10 watahitajika kumpigia kura mshiriki huyo au hao.

Washiriki wawili waliotolewa kwenye mashindano hayo, Watapata nafasi ya upendeleo kuingia kwenye fainali yaani Top 10 kwa kupigiwa kura.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...