Na Amiri kilagalila-Njombe
Askari  watatu  wa  jeshi  la  polisi  mkoani  Njombe  wamefariki  dunia leo  baada ya  kutokea  ajali  iliyohusisha  basi la  kampuni  ya  Sharoon linalofanya safari zake Njombe -Arusha na kuligonga gari la polisi lililokuwa mbele yake.

Kamishna msaidizi  wa  polisi  mkoa  wa  Njombe  Hamis  Issa  amethibitisha  kutokea  kwa  tukio  hilo  na kusema  basi hilo  lenye  namba namba T349 CXD  limegonga  gari la polisi lililokuwa  mbele  yake lenye  namba PT 3734  toyota land cruser na kusababisha vifo vitatu na  majeshuhi  tisa.

Kamanda  Issa  amesema majeruhi wanaendelea  na matibabu katika  hospitali  ya  kibena na askari  watatu wamefariki wakati wakipelekwa kwenye matibabu.

“Katika ajali hiyo majeruhi ambao walikuwa wamezidiwa zaidi ni watano,mmoja anayetambulika kwa jina la kijeshi namba H 1839 PC Dickson huyu amepata maumivu ya shingo na maumivu mengine mwilini,na amepewa rufaa ya kwenda Muhimbili na hawezi kupanda gari  labda usafiri wa ndege hivyo mpaka sasa hivi tunafanya utaratibu askari huyu aweze kusafirishwa kwa matibabu na taratibu zote za kumpeleka zimeshakamilika”alisema Kamanda Issa

kamanda  issa  amesema askari waliofariki   kwenye ajali hiyo  kuwa  ni  namba H 4401 Mariharus  Said Hamis mkazi  wa lindi, namba H 6802 pc Michael Muhando mkazi wa Geita na H7486 pc Henry Athmani  Soka mkazi wa  Arusha na Kilimanjaro.

Kwa upande  wake  mganga  mfawidhi  wa  hospitali  ya  mji  wa  Njombe dkt Alto Damas  Mtega amesema  wamepokea  majeruhi tisa na  miili mitatu  ambao wamefikishwa  kwaajili ya matibabu  majira  ya  saa kumi na mbili na  dakika 10

“Tumepata majeruhi leo ambao wametokana na ajari na wote walikuwa ni askari polisi ilikuwa ni saa kumi na mbili kama dakika kumi ,walikuwa wanatoka kituoni wanaelekea kazini,kwa hiyo tumepata jumla ya majeruhi 7 lakini pia watatu walikuwa wamepoteza maisha,jumla kwenye gari walikuwa watu kumi na mbili na wawili hali zao sio nzuri sana watahitaji kupewa rufaa”alisema Damas Mtega

Majeruhi wa ajali hiyo  Mustapha  Said  amesema  namna  ilivyotokea  hawezikuelezea kutokana  na  mshtuko  uliotokea  na kushindwa kuelewa namna ilivyokuwa.

“Tuliona tu gari imepigwa kwa nyuma na watu wote walikuwa wamesharuka kwa hiyo pale hatukuweza kutambua kitu chochote”alisema Mustapha Said

Miili ya  marehemu  hao inatarajiwa  kusafirishwa  kesho saa  saba mchana kuelekea  nyumbani  kwa marehemu hao  kwaajili ya  mazishi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...