Naibu Msajili
wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Ruth Massam (kushoto)
akiwakabidhi vitu mbalimbali wauguzi wa Taasisi ya Mifupa (MOI),
iliyopo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili wanaohudumia watoto
waliozaliwa na vichwa vikubwa ambao wanapata matibabu hospitalini hapo.
Afisa Ustawi wa
Jamii Mwandamizi kutoka katika taasisi hiyo, Bw. Frank Matua akitoa
taarifa fupi kuhusu watoto wanaozaliwa na vichwa vikubwa.
Hakimu
Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Mhe. Martha Mpaze akishusha
vitu mbalimbali vilivyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo
kwa ajili ya kusaidia watoto waliozaliwa na vichwa vikubwa wakiwemo
mama zao ambao wanapata matibabu katika Taasisi ya Mifupa (MOI),
iliyopo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili. Ikiwa ni moja ya huduma
waliyoifanya katika kuadhimisha Wiki ya Sheria ya mwaka huu.

Naibu Msajili
wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Ruth Massam (kushoto)
akitoa elimu ya sheria kwa wakina mama ambao wenye watoto waliozaliwa
na vichwa vikubwa ambao wanapata matibabu katika Taasisi ya Mifupa
(MOI), iliyopo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...