Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji Chogo ,Kamishna Msaidizi,Kennedy Komba(kulia) wakati wa ukaguzi wa mabweni yanayotumiwa na wanafunzi wa chuo hicho kilichopo wilayani Handeni mkoani Tanga,leo.Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(wapili kulia),Mkuu wa Wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe (watatu kulia),Mbunge wa Handeni Vijijini,Mboni Mhita(kushoto) na   Mkuu wa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji Chogo ,Kamishna Msaidizi,Kennedy Komba(kulia), wakipita katika moja ya mabweni yanayojengwa katika chuo wakati wa ziara ya naibu waziri leo kukagua ujenzi  wa mabweni  wilayani Handeni mkoani Tanga.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani),wakati wa kikao cha ndani kilichohusisha Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama baada ya naibu waziri kuwasili wilayani Handeni leo  kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Handeni,mkoani Tanga leo baada ya kuwasili katika kijiji cha Chogo kwa ziara ya kikazi.Kushoto ni Mkuu wa wilaya hiyo,Godwin Gondwe.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...