Na.Khadija seif, Michuzi Tv
WAUMINI wa dini zote watakiwa kuliombea Taifa la Tanzania ili kuepuka majanga .
Mtumishi
wa mungu Nabii Joshua Aram amesema wakati mwengine taifa linapofikwa na
majanga yanayohatarisha maisha ni muhimu waumini wote kuungana na kuwa
kitu kimoja ili kuliombea taifa kuepuka majanga na maafa .
"kwa
mwaka huu tumeshuhudia majanga ya moto kwenye station ya mafuta
kigamboni lakini kwa uwezo wa mungu tumeweza kuliepuka na madhara
hayakutokea hivyo basi tuone ni nafasi pekee ambayo mungu ametupa wasaha
wakumshukuru na kumuomba amani hata hivyo nchi ya china tumeendelea
kushuhudia ugonjwa wa virusi vya corona vikiendelea kuwasumbua tuombe
Sana mungu ugonjwa huo usifike nchini kwetu,"
Aidha,Joshua amesema watanzania wanatakiwa kuitumia amani kama tunu ili kujipatia maendeleo.
"amani
haiwezi kudumu pasipo kumuomba mungu aendelee kutujaalia amani hiyo
waumini wote tuungane tuombe mungu ili pasitokee mtu,kikundi
kitakachoweza kuvuruga amani hii tuliyoachiwa na mababu zetu,"
Hata
hivyo amempongeza Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania John pombe
Magufuli kwa kuendelea kutetea wanyonge na kuhimarisha uchapakazi hasa
kwa vijana.
"Magufuli ni
Kiongozi wa kipekee anaependa usawa kwa watu wote ndio maana anaitwa
rais wa wanyonge hivyo tumuunge mkono na tumuombee pia kwa maana kazi
anayofanya sio ndogo hasa linapokuja swala la kuliongoza Taifa,"


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...