Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MTOTO wa miaka 13 amefariki dunia nchini Uingereza mara baada ya kukutwa na maambukizi ya virusi vya Corona (Covid-19) hospitali King's College ya Mjini London na ndugu wa mtoto huyo wamevieleza vyombo vya habari.

Mtoto huyo raia wa Uingereza alifariki dunia siku ya Jumatatu ameelezwa kuwa ni muingereza mdogo zaidi kufariki kwa virusi hivyo.

Familia ya mtoto huyo imevieleza vyombo vya habari kuwa mtoto huyo (Ismail Mohamed Abdulwahab) alianza kuonesha dalili hasa katika kupata shida ya upumuaji kabla hajapelekwa hospitali.

"Aliwekwa katika mashine ya kumsaida kupumua baadaye akawa mahututi na alifariki siku iliyofuata asubuhi" ameeleza mmoja ya wanafamilia.

Mkufunzi wa chuo cha King's College Nathalie MacDermott amesema kuwa;
 
 "Wakati tukifahamu  ni nadra sana kwa watoto kupatwa na Covid 19 ukilinganisha na watu wazima, visa hivi vimeonesha umuhimu wa sisi sote kuchukua tahadhari ili kudhibiti kuenea kwa virusi hivi duniani kote" amesema.

Mapema jumanne kifo cha mtoto wa kike wa miaka 12 kilithibitishwa kuwa ni kifo cha mtu mdogo zaidi kutokea  nchini Ubelgiji.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...