Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

DEREK Chauvin ofisa wa polisi nchini Marekani amefahamika zaidi tangu Mei 25 mwaka huu na hiyo ni  baada ya kutekeleza mauaji ya mmarekani mweusi George Floyd hadharani kwa kumkandamiza shingo kwa takribani dakika nane hadi umauti ulipomkuta.

Derek Chauvin alizaliwa Machi 19, 1976 huko Fayetteville na alihamia  Minneapolis, Minnesota mwaka 2014 na alianza kufanya kazi akiwa ofisa wa polisi katika idara ya polisi Minneapolis mwaka 2001.

Kabla ya kufanya mauaji ya George, Derek amewahi kuwa na malalamiko 18 yaliyokuwa yakimkabili akiwa kazini ambapo baadhi ya  malalamiko yaliondolewa kwa kuonywa kinidhamu na kupewa barua za onyo.

Kati ya mwaka 2006 na 2011 taarifa za kiofisi zinaonesha kuwa Derek alikuwa na matukio ya matatu ya matumizi mabaya ya silaha likiwemo la kujeruhi kwa kisu kilichohusisha polisi 6 na  tukio jingine lilisababisha kifo.

Baada ya Derek kutekeleza tukio hilo mkewe Kelly Chauvin alilaani tukio hilo mbele ya vyombo vya habari na tayari ameshaanza mchakato wa kubadili jina la mwisho na kudai talaka kwa ndoa yao iliyofungwa June 12, 2010.

Aidha kwa mujibu wa aliyekuwa mmliki wa ukumbi wa El Nuevo Rodeo Maya Santamaria aliieleza CNN kuwa Derek na George walikuwa wakifanya kazi ya ulinzi katika ukumbi huo ambapo George alifanya kazi ya ulinzi siku ya Jumanne kama mlinzi wa ziada na Derek alifanya kazi hiyo kwa muda wa ziada akiwa polisi katika ukumbi huo kwa takribani miaka 17.

Hakuna ndugu wa Derek anayefahamika isipokuwa mkewe Kellie Chauvin, na imeelezwa kuwa  Derek hapatikani katika mitandao ya kijamii kama Facebook, Instagram, Twitter na YouTube.

Derek ameharibu kazi yake kwa dakika nane pekee, ni kazi aliyoitumikia kwa miaka ipatayo kumi na minane licha ya kuwa barua za maonyo na malalamiko ya kinidhamu kumi na nane na yaliyokuwa yakimkabili.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...