Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Amon Mpanju(kulia) leo ametembelea Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Kigoma ili kujionea hali ya utoaji huduma ya haki kwa wananchi hususan wanyonge, ikiwemo ya Msaada wa Kisheria kabla ya uzinduzi wa Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria Mkoa wa Kigoma. Aidha Mpanju amefanya mazungumzo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ilvin Mugeta(kushoto) ambaye alimwelezea ubora wa huduma inayotolewa katika Mahakama hiyo kupitia Mahakama Mtandao na kuhusu kutoa ofisi kkutoka jengo hilo kwa ajili ya huduma ya msaada wa kisheria. (Picha na Festor Sanga- Mahakam, Kigoma)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...