TAKUKURU MANYARA YAWAPA ONYO VIONGOZI WA CCM WANAOKATA MAJINA
Na Mwandishi Wetu, Babati
MKUU
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Manyara
Holle Joseph Makungu amewaonya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
ambao wanaondoa majina ya wapiga kura halali wa kura za maoni na
kubandika majina ambayo wanaamini watawapigia kura wagombea ambao
wanawataka.
Makungu
ameyasema hayo mjini Babati Julai 16 baada ya kupata taarifa kwamba
baadhi ya viongozi wa chama hicho tawala ngazi ya kata wamekuwa na
mtindo huo jambo ambalo ni kinyume na taratibu.
Amesema wamesambaza makachero wa TAKUKURU kufanya uhakiki wa majina halali kwenye maeneo yanayolalamikiwa.
Amewaambia
viongozi wa CCM wanaofanya mabadiliko hayo, wafahamu kuwa hawako juu ya
sheria na kwamba kitendo hicho cha kubadilisha majina ya wapiga kura ni
kosa la kughushi ambalo likithibitishwa adhabu yake kwa mujibu wa
Kifungu cha 337 kanuni ya adhabu ni miaka saba jela.
"Makosa
ya rushwa katika kipindi cha uchaguzi yameanishwa katika vifungu vya
21, 22 na 23 vya sheria ya Gharama za uchaguzi namba 6/2010 ambavyo ni
pamoja na hongo ya fedha kwa wapiga kura ili kuwashawishi kupiga au
kutopiga kura , ahadi za ajira kwa wapiga kura kwamba nitakuajiri kwenye
ofisi fulani, kutoa zawadi, mikopo isiyo na riba au riba iliyo kinyume
cha sheria," amesema Makungu.
Amesema
makosa hayo pia yanamhusu mpiga kura anayekubali kupokea fedha,zawadi,
mikopo, ahadi ya ajira au kitu chochote cha thamani ili ampigie kura au
asipige kura kwa mgombea.
Ameongeza
kuwa ni kosa pia kutoa vyakula, vinywaji kwa nia ya kushawishi wapiga
kura, sheria ambayo inaanza kufanya kazi kuanzia wakati wa mchakato wa
wagombea ndani ya vyama vyote vya siasa hadi wakati wa uchaguzi mkuu
hapo Oktoba 2020.
Ametoa
onyo kwa Viongozi hao wa kata warejeshe majina ya wapiga kura za maoni
ambao ni halali mara moja na kuwataka makatibu wa wilaya wa chama cha
Mapinduzi kutoa ushirikiano kwa makachero wao wanaoshugulikia uchunguzi
huo kubaini wachache wanaotaka kurejesha demokrasia nyuma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...