Na Karama Kenyunko Michuzi TV. 
MKAZI wa Arusha eneo la Wakingori Kisimiri Chini, Kaaneli Akyoo (50) amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha akikabiliwa na shtaka moja la kusafirisha dawa za kulevya 

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na upande wa Jamuhuri mbele ya Hakimu Mushi imedai kuwa mshtakiwa ametenda kosa hilo Agosti 19, mwaka 2020 huko katika kijiji cha Kisimiri chini wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Inadaiwa kuwa siku ya tukio mshtakiwa Akyoo alikutwa akisafirisha dawa za kulevya aina ya bangi zenye uzito wa kilograms 160 huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa na kinyume cha sheria.

Hata hivyo, mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande hadi Septemba 7, 2020 kesi hiyo itakapokuja kwa ajili ya kutajwa. Kwa mujibu3wa upande wa Jamuhuri upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...