Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Chato

KAMPENI za mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)zimeingia mzunguko wa pili kwa kishindo baada ya mgombea wake Dk.John Magufuli kufanya mkutano katika wilaya ya Chato mkoani Geita na kuhudhuria na maelfu ya wananchi.

Katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo Septemba 14,2020 katika viwanja vya Mazaina wilayani hapa, Dk.Magufuli ametumia nafasi hiyo kuelezea mipango na mikakati ambayo yeye na Chama chake wanakwenda kuitekeleza iwapo watapata ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mingine mitano ijayo baada ya kufanya kazi kubwa ya maendeleo kwa miaka mitano iliyopita.

Dk.Magufuli alikuwa katika mapumziko ya siku tano wilayani hump tangu Septemba 9 mpaka leo Septemba 14 mwaka huu.Akizungumza zaidi kuhusu kampeni Dk.Magufuli amesema baada ya kufanya kazi ya kuleta maendeleo kwa mafanikio makubwa kwa kushirikiana na Watanzania wote sasa anarudi tena kuomba ridhaa kwa mara nyingine tena ili aendelee kuwatumikia na kuleta maendeleo zaidi .

"Hapa Chato watoto wengi walikuwa hawaendi shule, wakati nasoma tulioenda sekondari tulikuwa wawili, sio kwamba wale waliokosa nafasi ya kwenda sekondari hawakuwa na akili, walikuwa nazo lakini shule zilikuwa hazitoshi. Tukaamua kutafuta fedha ili watoto wasome , tukabana mafisadi na watoto wanasoma bure

 "Katika kipindi cha miaka mitano Sh.trilioni 1.09 kwa ajili ya kutoa elimu bure, lakini Sh.bilioni 450 kwa ajili ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu, lengo ni kuhakikisha Taifa hili linakuwa na watu waliosoma,"amesema 

Dk.Magufuli amesema kutokana na maendeleo waliyoyafanya wilaya ya chato imeweza kuwa na maendeleo zaidi hata ukiangalia shule ya chato kwa sasa hadi imezungushiwa ukuta.

Ameeleza namna ambavyo Serikali imefanha mambo makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu ya barabara,maji, afya, usafiri wa anga,usafiri wa anga,usafiri wa majini katika maziwa makuu, ujenzi wa madara makubwa na madogo."Ndio maana tunakuja tena kuomba ridhaa mtupe tena miaka mitano."

Akimzungumzia Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chato,Dkt.Melard Kalemani amesema alimwambia huenda usionekane jimboni kutokana na majukumu aliyompa ya kusimamia Wizara ya Nishati nchini na amefanya kazi nzuri na amekuwa akifanya kazi nchi zima.

Amesema alishangaa walipoona watu 60 kuchukua fomu za kugombea Ubunge." Tunahitaji watu wanaofanya kazi  na wala hatuchagui sura hivyo wanachato mchagueni kalemani kwa kura nyingi  ili akasimamie miradi ambayo anayoijua.

"Msidanganywe na watu wanaokaa vijiweni,mnataka akawe anasafisha viatu na kunywa kahawa,"amehoji.Aidha amemuagiza Dkt.Kalemani kupeleka mataa ya Barabarani katika jimbo la Bukombe.

Amesema mafanikio yote yanayofanywa na serikali ni kutengeneza maisha ya baadae ya watoto, kwani inawezekana  kwa umri wao wasifaidi hayo,ila kwa miaka ijayo ikawa inamanufaa kwa watoto wa vizazi vijavyo.
 Mgombea wa Urais kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wakati akiondoka katika viwanja vya Mazaina mara baada ya kuwahutubia wananchi wa Chato mkoani Geita.
 Mgombea wa Urais kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Chato

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...