Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amesisitiza ujio wa kipigo kikubwa kwa vyama vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 28 mwaka huu.

Ameyasema hayo tarehe 05 Oktoba, 2020 akizungumza na Wazee Kisiwandui Afisi Kuu Zanzibar.

"Jambo la msingi limetusaidia ni kuwa na wagombea ambao wanaweza kuanza na kufika mwisho wa kampeni ukilinganisha na vyama vingine, nimesikia kuna vyama vimeishiwa pumzi, wanaanza sasa kupanga hapa diwani awe wa chama kipi, maana wengine wapo chali, na wamefika mpaka ngazi ya Urais, wanawapumzisha wagombea fulani, ili waone upepo."

Akisisitiza uwezo wa CCM kushinda ameeleza,
"Hata wakihamisha pumzi kwa mmoja, kipigo kipo pale pale."

Katibu Mkuu akizungumza na wazee hao, licha ya CCM kuwa na uhakika wa ushindi mkubwa, amehoji utaratibu unaotumiwa na baadhi ya vyama vya upinzani kuunganisha nguvu baada ya wagombea wa vyama hivyo kuanzia ngazi za Udiwani, Ubunge na hata Urais kuanza kukata pumzi na kutoweza tena kuendelea na shughuli za kampeni.

Ameeleza kuwa, utaratibu unaotumika haujawahi kufanyika, na ni utaratibu unaodhihirisha wazi vyama hivyo kutokujiandaa na shughuli za kampeni, lakini kinachosikitisha ni vyama hivyo kuanza kujiandaa kulalamikia matokeo ya baada ya Uchaguzi tarehe 28 Oktoba, 2020 CCM itakapopigiwa kura za kutosha na kushinda kwa kishindo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...