Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Baraza la Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA.)


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

JAJI Mkuu wa Mahakama ya Tanzania  Prof. Ibrahim Hamis Juma ametoa pongezi nyingi kwa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa usimamizi wake madhubuti katika kutoa mafunzo mbalimbali ya kujengea uwezo wa kiweledi na kiutendaji kwa watumishi wa Mahakama Tanzania.

 Jaji Mkuu ametoa kauli hiyo wakati akizindua  baraza la 7 na semina elekezi kwa  wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto iliyofanyika Oktoba 7, 2020 Jijini Dar es Salaam.

  Jaji Mkuu  amesema kwamba, Chuo cha IJA chini ya Baraza la Uongozi kimeonyesha mfano mzuri kwa kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake hasa  katika  kusimamia na kutekeleza malengo, huku mafunzo mengi na bora yakifanyika chini ya usimamizi wa Chuo sehemu mbalimbali za Nchi.

  Amesema kuwa, kati ya mafunzo hayo ni yale ambayo yalifanyika kwa ajili ya kuwajengea uwezo  Maafisa wa Mahakama ili kuweza kukabiliana na mashauri ya uchaguzi, hiyo imekuja na sambamba kabisa na kipindi hiki ambacho Nchi yetu inaingia kwenye Uchaguzi Mkuu wa viongozi.

Aidha, aliongeza kuwa Chuo kimeendesha mafunzo mbalimbali.  Kati ya  mafunzo hayo ni pamoja  namna bora ya uendeshaji wa mashauri ya mtoto ambayo yalitolewa kwa zaidi ya wadau 1000 nchini, Kutokana na Sera ya Mafunzo ya mwaka 2019 Mahakama ya Tanzania imetoa Jukumu kwa IJA kuratibu Mafunzo yote endelevu kwa Watumishi wa Mahakama.

“Huu ni wakati wa IJA kujiimarisha ili Chuo kitoe Mafunzo kwa watumishi wa mahakama katika eneo la utoaji haki mtandao”  amesema hayo  Jaji Mkuu.

 Jaji Mkuu aliendelea kueleza kuwa Chuo kinaratibu mashrikiano na Taasisi mbalimbali ndani na nje ya  nchi kwa ajili ya kubadilishana uzoefu kwa watendaji wa mahakama.  Katika mashirikiano hayo imepelekea Majaji kutoka Nchi ya Ujerumani na Afrika ya Kusini kufanya ziara ya Mafunzo kwa Majaji wa Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...