Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki pamoja wakijadili masuala mbalimbali na wazalishaji wa saruji nchini kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na namna bora ya kukuza sekta ya ujenzi nchini kupitia saruji, kikao kilichofanyika Ofisi za Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), jijini Dar es Salaam.

Wakurugenzi wa kampuni 9 za saruji zikiwemo Dangote Cement, Camel Cement, Nyati Cement, Mbeya Cement, Kilimanjaro Cement, Maweni Cement, Tanga Cement, Lake Cement, Twiga Cement pamoja na Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) wakiwa katika kikao cha pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki wakijadili masuala mbalimbali na wazalishaji wa saruji nchini kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na namna bora ya kukuza sekta ya ujenzi nchini kupitia saruji, kikao kilichofanyika Ofisi za Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), jijini Dar es Salaam.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...