Warembo 20 kutoka Kanda 5  za mikoa ya Tanzania wanatarajia kuanza kambi ya mchuano wa Fainali za Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania tarehe 26 Novemba 2020 jijini D’salaam. 

Hatua za awali za mashindano haya ulianza mapema mwezi Februari mwaka huu, baadae mchakato ulisitishwa kidogo kutokana na janga la ugonjwa wa Corona ulioikumba nchi yetu pamoja na dunia kwa ujumla. 

Mchakato wa kuwapata washiriki 100 wa awali uliendelea mwezi Juni mara baada ya tishio la ugonjwa wa virus vya Corona kumalizika, ambapo mchujo wa washiriki 100 ulifanyika na kuwapunguza hadi washiriki 50. 

Washiriki 50 walipewa majukumu ya kufanya  na kuwasilisha majibu yake kwa Wajumbe wa Kamati ya Miss Tanzania ambao ndio walikuwa na jukumu la kudadisi na kuperuzi  majibu ya washiriki wote. 

Kati ya washiriki 50 ni washiriki 20 tu ndio waliopita katika mchakato huo, nao wameshajulishwa tayari kuhusu kuingia kambi ya Miss Tanzania mwisho wa mwezi Novemba. 

Majina ya washiriki hao pamoja na umri wao ni  kama ifuatavyo:-

1. PRISCA LYIMO  umri miaka 22

2. TAMIA HAKAM  miaka 19

3. JULIANA RUGUMISA miaka 23

4. REHEMA CUTHBERT miaka 21

5. YVONNE PAUL miaka 20

6. RUTH BENITHO miaka 23 

7. GRACE MACHIBULA miaka 24

8. ROSE MANFERE miaka 20

9. MARGARET MWAMBI miaka 23

10. SARAFINA MAGEYE miaka 20

11. MARTHA GOLODI miaka 23

12. ZENITHA CHUNDU miaka 22

13. DEOLYN MOLLEL miaka 21

14. HOYCE BAKANOBA miaka 20

15. NECERIAN KIVUYO miaka 20

16. RAZIA ABRAHAM miaka 19

17. ANGELA PENDAELI miaka 23

18. ADVERA MWEMBA miaka 21

19. VERYNICE DEOKARI miaka 24

20. GLORIA FELA miaka 23

Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania yanaandaliwa na Kampuni ya The Look chini ya Mkurugenzi wake Bi. Basilla Mwanukuzi Shayo. Miss Tanzania 1998. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...