Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma (kulia) akimsikiliza Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Kesi Masalia za Mauaji ya Kimbari ‘IRMCT’, Bw. Abubacarr Tambadou. Bw. Tambadou ambaye alichaguliwa rasmi Julai mosi, 2020 amemtembelea Mhe. Jaji Mkuu kwa lengo la kujitambulisha na kuimarisha uhusiano.

Mazungumzo yakiendelea, kushoto ni Bi. Tully Mwaipopo, Mwanasheria kutoka Mahakama hiyo.

Picha ya pamoja.

Na Mary Gwera, Mahakama

MSAJILI wa Mahakama ya Kimataifa ya Kesi Masalia za Mauaji ya Kimbari ‘IRMCT’, Bw. Abubacarr Tambadou ameahidi kuendeleza ushirikiano wa utendaji kazi baina ya Mahakama hiyo na Mahakama ya Tanzania.

Akizungumza wakati alimpotembelea Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ofisini kwake leo Desemba 02, 2020, Msajili huyo alisema kuwa yupo tayari kuendeleza kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na ‘IRMCT’ kwa maslahi ya Taifa.

 “Nina furaha kukubali ombi langu la kuonana na wewe licha ya kuwa na majukumu mengi ya kazi, lengo la mimi kuja kukutembelea ni kujitambulisha rasmi na kuomba kuendeleza ushirikiano wa kikazi baina yetu,” alieleza Bw. Tambadou.

Vilevile, Bw. Tambadou alieleza kuwa Mahakama ya Tanzania itumie vyema uwepo wa Mahakama ya Kimataifa ya Kesi Masalia za Mauaji ya Kimbari ‘IRMCT’ kama tija ya kujua zaidi sheria za kimataifa.

Naye, Mhe. Jaji Mkuu alimuahidi Msajili huyo kutoa ushirikiano zaidi na kuahidi kumtembelea pindi atakapokuwa Arusha.

Aidha; Mhe. Jaji Mkuu alipataa wasaa wa kumueleza Msajili huyo kuwa Mahakama ipo katika maboresho mbalimbali yanayolenga kurahisisha na kusogeza huduma za haki karibu zaidi na wananchi.

Hali kadhalika Mhe. Jaji Prof. Juma alimueleza Bw. Tambadou kuwa Mahakama ya Tanzania kwa sasa ipo katika maandalizi ya kuadhimisha miaka 100 ya kuanzishwa kwa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Bw. Abubacarr Tambadou alichaguliwa kuwa Msajili wa Mahakama hiyo Julai mosi mwaka huu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...