Na Mwaandishi Wetu Mtwara

KIWANDA cha Saruji cha Dangote Mkoani Mtwara kinatarajia kujenga kituo chake cha pili cha gesi asilia (CNG-Compressed Natura Gas) katika mkoa wa Dar es Salaam ambacho kitatumika kutoa gesi safi, salama na kwa gharama ya chini kwa malori yanayosafirisha saruji kwenda sehemu mbalimbali nchini.

Hivi karibu kiwanda hicho kilizindua kituo cha kwanza kilichopo kiwandani Mkoani hapa (Mtwara) chenye uwezo wa Mita za Ujazo 5000 kwa saa (sawa na lita 5000 za mafuta [Automated Gas Oil]). Kituo hicho kitatumika  kutoa gesi safi, salama  na kwa gharama ya chini  kwa takribani malori  250.

Waziri wa Nishati Medard Kaleman alizindua  kituo hicho na kuwapongeza uongozi wa kiwanda cha Dangote kwa uwekezaji wa kituo hicho cha CNG.

Akizungumza katika hafla ya kuzindua kituo hicho Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Dangote Engineer Abdullahi Baba alismea  malori hayo yamebadilishwa kuweza kutumia mifumo miwili yaani AGO (mafuta) na CNG (gesi asilia) kwa wakati mmoja.

“Pamoja na hayo uwezo, wa kituo hicho  utatosha kusaidia  katika mkakati wa kampuni juu ya matumizi ya mafuta hapo baadae  ambao pia utahusisha  matumizi ya gesi asilia katika malori  kwa asilimia 100 katika safari zake zote,” alisema.

Akizungumzia kiwanda ambacho kitajengwa Dar es Salaam Baba alisema Kituo hicho kitajengwa jijini Dar es Salaam umbali wa kilomita 550 kutoka  kilipo kiwanda cha saruji cha Dangote.

Aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira mazuri ambayo yamevutia kiwanda hicho cha Dangote kuweza kuwekeza kwenye sekta ya gesi huku.

 “Kwa mara nyingine  tena kiwanda cha Dangote  kimefungua njia katika soko kupitia  utekelezaji wa teknolojia hii  huku kikipata msaada mkubwa  kutoka kwa serikali ya Tanzania, na kwa  sasa kiwanda cha Dangote kimejipanga kuwa  watumiaji wa kubwa wa pili  wa gesi asilia  nchini baada ya TANESCO,” alisema.

Alisema Tanzania ni kama Nigeria, imejaaliwa  akiba kubwa ya gesi asilia  ambapo  matumizi ya gesi hii katika magari  yana manufaa makubwa   kifedha na kimazingira.

“Nataka niwahakikishie Dangote na wale wengine wenye nia kutumia rasilimali ya gesi katika magari, serikali ipo pamoja na nyinyi kuhakikisha kwamba inaweka na kujenga mazingira wezeshi ili kaiz yah ii iwe endelevu,” alisema Waziri Kaleman.

Waziri wa Nishati Medard Kaleman (wa pili kulia) akizindua kituo cha kwanza cha kusindika gesi asilia kwenye malori ya Kiwanda hicho cha Dangote Mtwara. (Wa kwanza kulia ni Mkurungezi wa TPDC Dr James Mataragio na wa tatu ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa
Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Dangote Engineer Abdullahi Baba akitoa hotuba katika hafla ya kuzindua kituo chao cha kwanza cha kusindika gesi asilia kwenye mabasi Yao yanayosafirisha Saruji kwenda mikoani

Mtambo wa kusindika gesi asilia kwenye malori

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...