NA MWAMVUA MWINYI,PWANI


MKOA wa Pwani ,umepitisha rasimu ya mapendekezo ya mpango na bajeti wa mwaka 2021/2022 ,ya kiasi cha sh.bilioni 298 ikiwa ni ongezeko la sh .bilioni 25 sawa na asilimia 9 kutoka katika bajeti ya mwaka 2020-2021 ya sh.bilioni 272.

Kufuatia ongezeko hilo ,sekretarieti ya mkoa imezisihi halmashauri za wilaya na mji kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato pamoja na kutafuta vyanzo vipya vya mapato ya ndani.

Akiwasilisha rasimu hiyo ya mapendekezo ,kwenye kikao cha ushauri cha mkoa wa Pwani (RCC),Mchumi wa mkoa huo Gerald Mbosoli alisema, zipo halmashauri ambazo hazijafikia asilimia 50 hadi kufikia Desemba mwaka jana hivyo anaamini kufikia June mwaka huu malengo  yatafikiwa.

"Ila katika utekelezaji wa bejeti inayomalizika kulikuwa na changamoto ya upungufu wa vitendea kazi ,watumishi na raslimali fedha hazitoshelezi kulingana na uhalisia." alielezea Mbosoli.

Mbosoli alieleza, ipo mikakati waliyojiwekea ikiwa ni pamoja na uboreshaji katika huduma za jamii na kusanyaji wa mapato .

Alifafanua kwamba, maeneo mengine ni usimamizi wa stahiki za wananchi na maeneo yaliyopewa vipaombele na ni mtambuka ikiwemo VVU ,lishe .

Akifunga kikao hicho mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo alizitaka halmashauri kuongeza juhudi za kusimamia makusanyo na kufuatilia mianya ya upotevu wa mapato ili kuinua mapato yao.

Akizungumzia hoja iliyoibuka kutoka wilaya ya Mafia juu ya mapato makubwa kuelekea jiji la Ilala ,alisema baharini hakuna vizuia ,lakini zipo halmashauri zinazoumia kutokana na sheria zilizopo.

Akichangia agenda hiyo, mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mafia ,Erick Mapunda alisema kuwa wana changamoto kubwa ya mapato ya wavuvi wadogo kulipiwa jiji la Ilala.

"Wapo wavuvi wadogo kutoka Dar es salaam ambao wamekuja Mafia na kutumia eneo letu kuvua na kuondoka kujipatia soko Dar es salaam ,hawa wamekuwa wakikataa kulipia ,hali inayosababisha halmashauri yetu kukosa mapato makubwa kutoka kwao ,"

Mapunda aliziomba mamlaka husika zinazosimamia masuala ya aina hiyo ,kuliona tatizo hilo na kuishauri serikali kufanya mabadiliko ya ulinzi kwani yana athiri halmashauri zinazopakana kwa bahari ama ziwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...