Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Songea Mjini , Dkt. Damas Ndumbaro akikata utepe  wakati akizindua rasmi msimu wa saba wa Tamasha la Majimaji Selebuka litakalofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 31 Julai  kwenye Viwanja vya Maji Maji Songea mkoani Ruvuma. Wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Songea, Mhe. Pololet Mgema akiwa na  Viongozi  wengine  wa Kiserikali na Taasisi za Misitu nchini.
 
 
======  =======  =========
Waziri wa Maliasili  na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro ameziagiza Taasisi zote za Wizara ya Maliasili na Utalii ambazo zinatangaza Utalii na zinafanya Uhifadhi kuweza kushiriki Tamasha la Majimaji Selebuka.
 
Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika mkoani Ruvuma  kuanzia tarehe 24 Julai hadi 31 mwaka huu katika Uwanja wa Majimaji Songea likiwa na lengo la kuhamasisha utalii wa ndani, michezo pamoja na kukuza na kuenzi utamaduni wetu.
 
Ametoa agizo  hilo wakati  akizindua msimu wa saba la Tamasha hilo uliofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia 24 na 25 Aprili katika Viwanja vya Makumbusho ya Majimaji  ikiwa ni maandalizi ya Tamasha lenyewe litakalofanyika mwezi Julai  kwa muda wa siku saba mkoani hapo.Katika Tamasha hilo ambalo kwa mwaka huu limebeba kauli mbiu isemayo ” Misitu ni Uchumi ” Dkt.Ndumbaro amesema kwa mwaka huu Tamasha linatoa hamasa kwa  Jamii  kutunza misitu zaidi.
 
Waziri Dkt. Ndumbaro amesema anategemea Tamasha hilo kwa mwaka huu litakuwa kubwa sana na litatoa fursa kwa Watu mbalimbali  kuanza kutembelea  vivutio mbalimbali vya Utalii ambavyo vipo mkoani Ruvuma likiwemo Pori la Akiba LipalambaKatika hatua nyingine, Amemuomba Mkuu wa  Wilaya ya Songea  kutumia mamlaka yake ya kuzitaka Taasisi zilizo katika wilaya yake kushiriki katika Tamasha hilo.
 
 ‘” Mkuu wa wilaya najua una Taasisi nyingi sana katika wilaya yako ninakuomba na ninaamini una Mamlaka hiyo, toa maelekzo kwa Taasisi zote zinanazotoa huduma na kufanya biashara zishiriki Tamasha la Majimaji Selebuka ” alisisitiza Waziri Dkt.Ndumbaro Aidha amezitaka Halmashauri ya Songea pamoja Halmashauri zingine ziweze kushiriki Tamasha hiloAidha, Waziri  Dkt. Ndumbaro  ametumia fursa hiyo kuziomba Taasisi nyingine za Watu binafsi kushiriki katika Tamasha hilo ili ziweze kutoa huduma kwa jamii katika msimu wa Tamasha hilo.
 
Kwa upande wake Mratibu wa Tamasha hilo Reinfrida Rwezaura, amesema Tamasha hilo tangu kuanzishwa kwake limekuwa ni Jukwaa bora kwa kuwakutanisha Wafanyabiashara, Wajasiliamali, wanamichezo, wanafunzi, na wadau mbalimbali katika kuendelea kuutangaza uchumi na utalii nchini Waziri wa Maliasili  na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro ameziagiza Taasisi zote za Wizara ya Maliasili na Utalii ambazo zinatangaza Utalii na zinafanya Uhifadhi kuweza kushiriki Tamasha la Majimaji Selebuka.
 
Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika mkoani Ruvuma  kuanzia tarehe 24 Julai hadi 31 mwaka huu katika Uwanja wa Majimaji Songea likiwa na lengo la kuhamasisha utalii wa ndani, michezo pamoja na kukuza na kuenzi utamaduni wetu.
 
Ametoa agizo  hilo wakati  akizindua msimu wa saba la Tamasha hilo uliofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia 24 na 25 Aprili katika Viwanja vya Makumbusho ya Majimaji  ikiwa ni maandalizi ya Tamasha lenyewe litakalofanyika mwezi Julai  kwa muda wa siku saba mkoani hapoKatika Tamasha hilo ambalo kwa mwaka huu limebeba kauli mbiu isemayo ” Misitu ni Uchumi ” Dkt.Ndumbaro amesema kwa mwaka huu Tamasha linatoa hamasa kwa  Jamii  kutunza misitu zaidi.
 
Waziri Dkt. Ndumbaro amesema anategemea Tamasha hilo kwa mwaka huu litakuwa kubwa sana na litatoa fursa kwa Watu mbalimbali  kuanza kutembelea  vivutio mbalimbali vya Utalii ambavyo vipo mkoani Ruvuma likiwemo Pori la Akiba LipalambaKatika hatua nyingine, Amemuomba Mkuu wa  Wilaya ya Songea  kutumia mamlaka yake ya kuzitaka Taasisi zilizo katika wilaya yake kushiriki katika Tamasha hilo.
 
 ‘” Mkuu wa wilaya najua una Taasisi nyingi sana katika wilaya yako ninakuomba na ninaamini una Mamlaka hiyo, toa maelekzo kwa Taasisi zote zinanazotoa huduma na kufanya biashara zishiriki Tamasha la Majimaji Selebuka ” alisisitiza Waziri Dkt.Ndumbaro 
Aidha amezitaka Halmashauri ya Songea pamoja Halmashauri zingine ziweze kushiriki Tamasha hilo
 
Aidha, Waziri  Dkt. Ndumbaro  ametumia fursa hiyo kuziomba Taasisi nyingine za Watu binafsi kushiriki katika Tamasha hilo ili ziweze kutoa huduma kwa jamii katika msimu wa Tamasha hilo.Kwa upande wake Mratibu wa Tamasha hilo Reinfrida Rwezaura, amesema Tamasha hilo tangu kuanzishwa kwake limekuwa ni Jukwaa bora kwa kuwakutanisha Wafanyabiashara, Wajasiliamali, wanamichezo, wanafunzi, na wadau mbalimbali katika kuendelea kuutangaza uchumi na utalii nchini 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...