kushoto ni mkuu wa wilaya mpya wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo akikabidhiwa na mkuu wa wilaya aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo Richard Kasesela ilani ya CCM ambayo na yeye alikabidhiwa na chama cha mapinduzi alipokuwa mkuu wa wilaya hiyo kabla ya kutenguliwa uteuzi wake
kushoto ni mkuu wa wilaya mpya wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo akikabidhiwa na mkuu wa wilaya aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo Richard Kasesela nyaraka za wilaya hiyo ambayo na yeye kwa lengo la kuijua vizuri wilaya hiyo.
Na Fredy Mgunda,Iringa.
MKUU mkuu wa wilaya ya Iringa
ametakiwa kuhakikisha anatatua changamoto ya migogoro ya ardhi ambayo imekuwa
gumzo katika wilaya hiyo kutokana na wananchi wa wilaya kuuza ardhi mara
mbilimbili na kuvamia baadhi ya ardhi za wawekezaji zenye hati miliki za miaka
mingi ya nyuma.
Akizungumza wakati wa kukabidhi
ofisi ya mkuu wa wilaya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Iringa Richard
Kasesela alisema kuwa wailaya hiyo
imekuwa na migogoro mingi ya ardhi ambayo mara kadhaa imekuwa ikisababishwa na
wananchi wenyewe.
Alimuomba mkuu wa wilaya mpya
kuhakikisha kuwa anakuwa makini namna ya kutatua migogoro hiyo kutokana na
asili ya wananchi wa wilaya hiyo kwa namna ambavyo wanaishi na kutengeneza
migogoro hiyo ambayo imekuwa ikirudisha nyuma juhudi za maendeleo.
Kasesela alisema kuwa licha ya
kuwa wilaya hiyo kuna migogoro mingi lakini kuna fursa kubwa kwa wawekezaji
kuwekeza kwenye wilaya hiyo ambayo inautajili mkubwa ambao unaweza kukuza
uchumi wa wananchi wa wilaya hiyo.
Aliongeza kuwa wilaya hiyo ndio
kitovu na dira ya mkoa wa Iringa hivyo
anapaswa kuwa makini katika namna ambayo anaweza kuongoza kwa kuleta maendeleo
na kukuza uchumi wa wilaya hiyo ambayo kwenye sekta ya michezo hasa mpira wa
miguu ambao ndio umekuwa pendwa kwa wananchi wengi wa wilaya hiyo.
Kasesela alisema kuwa wilaya
hiyo imekuwa na miradi mingi ya kimaendeleo ambayo inahitaji kusimamiwa kwa
umakini ili kufikia lengo la miradi hiyo kuleta maendeleo kwa wananchi na
wilaya hiyo.
Alimalizia kwa kumpongeza mkuu
huyo wa wilaya kuteuliwa na kumuambia kuwa wananchi wa Iringa wanataka
kuheshiwa na kujali muda katika juhudi za kufanya maendeleo,isipokuwa hivyo
atapokea majungu mengi ambao yatasababisha migogoro.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya
ya Iringa,Mohamed Moyo alisema kuwa ameanza kuitatua baadhi ya migogoro ya
ardhi ambayo imekuwa inarudisha nyuma maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo.
Alisema kuwa anaomba
ushirikiano mkubwa kutoka kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo ili kuhakikisha
kuwa anafanikisha kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa kiuchumi na kukuza maendeleo
kwa wananchi wa wilaya hiyo kwa kuanzia pale mkuu wa wilaya aliyenguliwa nafasi
hiyo.
Moyo alisema kuwa ametokea
kwenye chama na yupo tayari kuhakikisha anatekereza vilivyo ilani ya chama cha
mapinduzi vilivyo ili kuleta maendeleo kwa wananchi wa wilaya ya Iringa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...