Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge amekutana na Wananchi wa Vijiji vya Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo, ambao wanalalamikia kutolipwa Fidia baada ya kuwepo Mchakato wa Ujenzi wa Barabara ya Afrika Mashariki, Makurunge, Saadani Tanga.

Kunenge ameeleza kuwa Awali Tathimini ya Fidia kwa Wanachi hao ilifanyika mwaka 2019 na malipo yamefanyika kwa Wananchi Pangani Tanga.

Jambo lilowatia hofu Wananchi hao ni kufanyika kwa Tathimini mpya ambayo fomula iliyotumika ni tofauti na ya mwaka 2019,hivyo kuwepo kwa Tathimini mbili kwenye mradi huo mmoja, na wakati huo huo Wananchi wa Vijiji Jirani wamelipwa kwa Tathimini ya awali.

"Mtalipwa Fidia kama walivyolipwa wenzenu wa Tanga, kwasababu ya Mazingira ya suala lenyewe kwamba Mradi ni mmoja Tathimini ilikwisha fanyika kilichofanya msilipwe kipindi hicho ni kukosekana kwa fedha" alisema Kunenge.

"Nimelichukua tutaenda kushauriana na Wizara fidia zilipwe kupitia vigezo walivyotumia kulipa wananchi wa Vijijini Jirani na kama inavyonekana kwenye Tathimini ya awali. Tutatumia hekima pia kutafutia ufumbuzi suala hilo alieleza Kunenge."vuteni subira suala hili tunalishughulikia"alisisitiza Kunenge.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge akizungumza na Wananchi wa Vijiji vya Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo leo Agosti 3,2021.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...