Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge amesema ,uongozi wa mkoa unatarajia kuanza ziara ya kata kwa kata ,lengo likiwa ni kusikiliza kero ,na kutembelea miradi ya kimkakati iliyopo mkoani hapo.

Aidha mkuu huyo ,amedhamiria kuvalia njuga kero kubwa ya migogoro ya ardhi ambapo baadhi  imeshaanza kutatuliwa kupitia kampeni ya ondoa migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na Waziri wa ardhi.

Kunenge aliyaeleza hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Pwani , kufahamiana na kujiwekea malengo ya mpango kazi Ili  kuutangaza Mkoa wa Pwani .

Alieleza ,hatua iliyopo sasa ni wataalam wa mkoa wapo katika maeneo mbalimbali kisha itapangwa ratiba rasmi ya ziara hiyo ambapo wataambatana na jopo la waandishi wa habari.

Hata hivyo,alisisitiza ushirikiano na Waandishi wa habari na kuwaomba kuwa wamoja ili kuutangaza mkoa huo ambao umesheheni viwanda,miradi mikakati ikiwemo reli ya kisasa SGR,Mradi mkubwa wa umeme Rufiji-Stigo na vivutio vya utalii .

"Bado kuna gap ,mkoa haujatangazika ipasavyo, kuna viwanda vikubwa ,vivutio vya utalii Saadan,Mafia lakini bado !!naomba tushirikiane watanzania wajue yaliyomo ndani ya mkoa huu "alifafanua Kunenge.

Nae Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Mhandisi  Mwanasha Tumbo ,alisema wataalamu wapo katika wilaya mbalimbali wakimalizia kufanya tathmini zilizoelekezwa ili kuanza ziara ya kata kwa kata.

Kwa upande wake mwandishi wa habari kutoka nipashe Julieth Mkireri ,alishukuru kuwepo kwa mkutano huo na kusema unakwenda kuleta umoja na kutimiza malengo ya mkoa.

Alieleza jukumu letu ni kuelimisha,kuhabarisha hivyo tutautangaza vema mkoa kama ilivyo kawaida ya majukumu yetu ya kikazi.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...