Na Linda Shebby
KAMISHNA
Msaidizi Muandamizi Mtaafu wa Jeshi la Polisi nchini SACP Jamal
Rwambow leo amezindua kitabu chake Kinachokwenda kwa jina Jamal Rwambow
kinachozungumzia maisha ya Kachero wa Polisi.
Akizungumza leo
katika uzinduzi huo ulio fanyika kwenye ukumbi wa mikutani uliopo
katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam alisema kuwa kitabu hicho
kitakua kikiuzwa kwa shilingi 25,000.
Aidha maudhui yaliyomo ndani ya kitabu hicho ni pamoja na historia iliyojaa mafunzo visa na mikasa ya ukachero.
"Katika kitabu hiki Kuna mambo mengi ya kujifunza vijana pamoja na makachero kwa ujumla" alisema SACP Rwambow.
Alisema
kuwa akipata msukumo wa kuandika kitabu hicho baada ya kung"amua kuwa
wapo watumishi wengi wakiwamo makamanda ambao wao wamefanya mambo
mengi makubwa na kuitumikia nchi lakini wamestaafu bila kufahamika
hivyo nimeandika kitabu hiki huku lengo kubwa likiwa ni kutunza
kumbukumbu,alisema Rwambow.
"Mimi ndiye niliweza kufanikiwa kukomesha
mauaji y watu wenye Ualbino wakati nilipokuwa Kamanda wa Mkoa wa Mwanza
(RPC), na nilifanikiwa baada ya kuweza kutumia mbinu zangu za kikachero
kwa kuwatumia wanajamii kupata taarifa mbalimbali ambapo niliokuwa
nikiwalipa kiasi Cha Mil1 huku aliyekuwa Mkuu wa Mkoa kwa kipindi kile
Hayati Abbas Kandoro aliongeza kiasi cha pesaSh. Mil.1 hivyo msamaria
mwema aliyeleta taarifa sahihi na Jeshi lilajiridhisha alikua akilipwa
kiasi cha Sh. mil 2.
Naye Mhandisi Filbert Rweyemamu ambaye ndiye
aliyeandika Dibaji ya kitabu hicho ametoa wito kwa maofisa na maaskari
ikiwemo raia kukinunua kitabu hicho kwa sababu Kuna mambo muhimu
wataweza kujifunza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...