Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

MABINGWA wa Kihistoria katika Soka la Tanzania, Young Africans SC wametwaa taji la Ngao ya Jamii 2021 baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba SC katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Bao pekee la Yanga SC lilifungwa na Mshambuliaji, Fiston Mayele dakika 11, baada ya kupokea asisti safi ya Winga, Farid Mussa Maliki aliyeichambua ngome ya Simba SC na kufanya mchezo huo kuisha ndani ya dakika 90 pekee.

 Katika kipute hicho Yanga SC walionekana bora zaidi katika eneo la Kiungo cha ukabaji kilichokuwa chini ya Yannick Bangala na Khalid Aucho wakiwalinda Mabeki wa kati, Bakari Nondo Mwamnyeto na Dickson Job.


Yanga SC imeanza msimu vyema msimu huu wa mashindano wa 2021-2022 baada ya ushindi huo ambapo Septemba 29, 2021 watafungua Pazia la Ligi Kuu Soka Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba wakati Simba SC wakifungua Ligi hiyo na Biashara United katika dimba la Karume mjini Musoma, Septemba 28, 2021.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...