Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

SIMBA SC wametupwa nje ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kupata matokeo ya jumla ya mabao 3-3 dhidi ya Jwaneng Galaxy FC ya Botswana kwenye mchezo wa mkondo wa pili uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, Simba SC walianza vyema na kupata bao la kuongoza kupitia Kiungo wake, Rally Bwalya kwenye dakika ya 41, wakati huo Jwaneng Galaxy FC walisawazisha bao hilo kupitia kwa Mchezaji Rudath Wendwell dakika ya 46 na 59 wakati bao la tatu likifungwa na Mchezaji Gape Mohutsiwa dakika ya 86.

Simba SC wanatupwa nje ya Michuano hiyo kwa bao la ugenini na kuruhusu mabao mengi nyumbani licha ya kupata mabao 2-0 nchini Botswana. Jwaneng Galaxy wanafuzu makundi ya Michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya matokeo hayo dhidi ya Wekundu wa Msimbazi.

Simba SC sasa inaangukia kwenye Michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF Confederations Cup) baada ya kutupwa nje kwenye raundi hiyo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...