Na Mwandishi Wetu, Vienna Nchini Austria

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Kusaya akiambatana na maafisa wengine ameiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa 64 wa Majadiliano ya Kamisheni ya Kimataifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya Duniani ulioanza Oktoba 18 - 21 Mwaka huu Jijini Vienna Nchini Austria.

Mkutano huo wenye lengo la kubadilishana uzoefu, kuimarisha ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa pamoja na kutatua changamoto zinazojitokeza katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Pia,  Mkutano huo  ulijadili namna bora ya kupambana na tatizo la dawa za kulevya na makosa mengine ya uhalifu wa kupangwa ikiwepo ya Ugaidi, Utakatishaji fedha, Usafirishaji haramu wa Binadamu na Uhalifu wa kimtandao na kuimarisha ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa pamoja nakutatua changamoto zinazojitokeza katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya Duniani


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...