Mechi ilikuwa ya aina yake ambapo kocha mpya wa Simba Sc alikuwa na kibarua kwenye mechi yake ya kwanza ya ligi na kufanikisha kuondoka na pointi tatu muhimu mbele ya maafande hao.
Katika mchezo huo Simba Sc ilianza kupata mabao matatu ya kuongoza katika kipindi cha kwanza kupitia kwa washambuliaji wao Kibu Dennis alifunga dakika ya 44 na Meddie Kagere ambaye amepachika mabao mawili dakika ya 17 na 36 kwenye mchezo huo.
Goli la kufutia machozi la Ruvu Shooting lilifungwa na Elias Maguli dakika ya 63.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...