Na Khadija Kalili, Kibaha
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakar Kunenge amewataka wakaazi wake kujitokeza katika kupata chanjo ya ugonjwa wa Uviko 19 kwa sababu  wanaoathirika zaidi na ugonjwa huo ni watu ambao hawajapata chanjo.
Alisema kuwa hivi sasa nchi imepata dozi aina tatu ambazo ni Pfizer, Sinopharm  na JJ  huku muhusika atakua huru kuchagua aina ya chanjo kati ya hizo.
RC Kunenge alisema hayo  leo Desemba 8 katika maadhimisho ya  kusherehekea miaka 60 ya Uhuru wa nchi katika maadhimisho yaliyofanyika kimkoa kwenye  Viwanja vya Mailimoja  Kibaha.

RC Kunenge alisema kuwa  maadhimisho haya yamefanyika kufuatia   maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa  kila Wilaya  na Mikoa  waaadhimishe sherehe hizo kimkoa huku kesho Desemba 9 itaadhimishwa kitaifa katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Aidha Kunenge amewataka wananchi Mkoani hapa kutulia majumbani mwao na kufuatilia kwa ukaribu matangazo ya maadhimisho ya ilele cha shereke za miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika  yatakayorushwa mubashara na vituo mbalimbali vya luninga huku  akiwaeleza kuwa wanapaswa kuziingatia  kuepuka misongamano isiyokuwa na ulazima ikiwa njia ya kuepuka maambukizi ya ugonjwa wa Uviko 19 ambao bado haujapatiwa dawa duniani kote.

Katika maadhimisho hayo  jambo lililovuta hisia za watu wengi ni kuwepo  kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha wa Kwanza na kuhudumu kwa miaka kumi yaani kati ya  mwaka 1978 hadi 1988 ambapo ni DC pekee aliyedumu kwa kipindi hicho  wakati  Wilaya hii ilipoanzishwa  aliyetambulishwa kwa jina la   Mary  Francis  Liwilo ambaye pindi alipopewa nafasi ya kuwasalimu wakaazi wa Kibaha alitoa historia ya  Wilaya hiyo ambayo iliwavutia wengi.
Aidha sherehe hizo za Mkoa zilipambwa na bendi ya Ruvu JKT

Pia Kikosi Cha Karate cha  Jeshi la Akiba  kilinogesha  sherehe hizo baada ya kuonyesha namna walivyoiva kimafunzo  ya Ulinzi na Usalama huku  wakiongozwa na mwanamama Rehema Dimwansi.

Wengine waluohudhuria  sherehe hizo ni pamoja na viongozi wa dini, watu mbalimbali katika Mkoa wa Pwani  pamoja na Kamati ya Usalama Wilaya na Mkoa kwa ujumla.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...