Na. Damian Kunambi, Njombe

Mahakama ya wilaya ya Ludewa iliyopo  mkoani Njombe imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Elias Mgaya (20) mkazi wa kijiji cha Madilu wilayani Ludewa mkoani Njombe kwa kosa la kumbaka bibi kizee wa miaka 70.

Akisomewa hukumu hiyo na hakimu Isaack Ayengo katika shauri namba 32 la mwaka 2021 Elias Mgaya ametiwa hatiani kwa kosa la ubakaji kinyume na kifungu cha 130 (1) (2)(c)na 131(1) Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya Sheria za Tanzania kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2019.

Awali akisomewa sitaka hilo na mwendesha mashtaka Asifiwe Asigile imeelezwa kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo machi 29  mwaka huu ambapo alimvamia bibi huyo(jina lake limehifadhiwa) nyakati za usiku akiwa amelala na kisha kutenda kosa hilo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...