Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 22 Desemba, 2021 ameshiriki Mkutano Maalum wa 18 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika kwa njia ya mtandao.

Mkutano huo Maalum umejadili ajenda kuu mbili ambazo ni kupokea ripoti ya Baraza la Mawaziri la Jumuiya hiyo ya uhakiki wa utayari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki na ajenda ya pili ilihusu pendekezo la mabadiliko ya Kanuni ya 11(1) inayohusu akidi ya Mikutano ya Wakuu wa Nchi na Wanachama wa Jumuiya hiyo.

Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo wamepokea taarifa ya uhakiki na kuagiza Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuharakisha mchakato wa majadiliano ya Mkataba (accession treaty) yatayowezesha DRC kuwa mwanachama na kuwasilisha taarifa hiyo katika mkutano wa kawaida utakaofanyika mapema mwaka 2022.

Aidha, kuhusu ajenda ya pili iliyohusu Kanuni ya 11(1), Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo wameagiza Baraza la Mawaziri la kisekta la Sheria na Mahakama kukutana ili kujadili kuhusu pendekezo la mabadiliko ya Kanuni ya 11 (1) ya uendeshaji wa Mikutano                     ya Wakuu wa Nchi Wanachama na kuwasilisha ripoti hiyo katika Mkutano ujao wa kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama kwa lengo la kujadili na kukamilisha suala hilo.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwa njia ya mtandao, Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamemkaribisha na kumpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa utendaji wake tangu ashike wadhifa huo.

Akihutubia kwa mara ya kwanza katika Mkutano huo, Mhe. Rais Samia amewashukuru Viongozi wa Jumuiya hiyo kwa ushirikiano mkubwa na kuahidi kuwa Tanzania itashiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki inatimiza malengo yake.

Aidha, Mhe. Rais Samia amesema Tanzania ikiwa kama mwenyeji wa Makao Makuu ya EAC, itahakikisha kuwa inatoa ushirikiano ili kuwezesha Taasisi hizo za Jumuiya kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Katika Mkutano huo wa EAC, Viongozi wa Jumuiya hiyo walisimama kwa dakika moja kumkumbuka Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa mchango wake alioutoa katika Jumuiya hiyo ya Afrika Mashariki.


Jaffar Haniu

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki Mkutano Maalum wa 18 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)uliofanyika kwa njia ya Mtandao leo tarehe 22 Desemba 2021 Ikulu Jijini Dr es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishiriki Mkutano Maluum wa 18 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika kwa njia ya mtandao leo tarehe 22 Desemba, 2021,  Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...