TPSF yaahidi ushirikiano na Serikali


Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

Serikali imesema kuwa itaendelea kuweka mazingira ya sekta binafsi ikiwemo kushiriki miradi ya kimkakati ili iweze kuinua wafanyabiashara nchini.

Hayo ameyasema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  wakati akifungua mkutano Mkuu wa 21 wa Taasisi ya Sekta Binafsi  Tanzania (TPSF) uliofanyika Jijini Dar es Salaam,amesema kuwa sekta binafsi inatakiwa kufanya kazi kwa kujituma ikiwa ni pamoja na kuweka fedha katika benki na sio kuzifungia ndani.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa kwa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Benki Kuu kuangalia namna ya kupunguza riba ili kufanya biashara ziweze kukua pamoja na kubaki na fedha za kuendesha biashara hiyo.

Amesema kuwa vitu vilivyokuwa vikwanzo wameweza kuondoa tozo ikiwa ni nia ya serikali kuhakikisha  sekta binafsi inakua kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Aidha amesema kuwa katika kufanya biashara kwa sekta binafsi waende kuwekeza hadi maeneo ya vijijini kutokana na serikali kuweka huduma ambazo ni wezeshi kwa kufanya biashara.

Hata hivyo Waziri Mkuu  ameziagiza Wizara ya Nishati na Wizara ya Maji kuhakikisha wanapeleka huduma za maji na nishati kwa maeneo yanayowekeza ili isiwe kikwazo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Taasisi za Udhibiti TBS,TMDA ,Ardhi kuwa na dirisha la pamoja katika ofisi za mikoa katika kurahisisha kuondoa usumbufu kwa wawekezaji pindi wanapotaka kuwekeza.

Nae Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Angelina Ngalula amesema kuwa serikali isaidie kuwashika mkono wafanyabiashara  kuweza kufanya biashara ndani na nje ya nchi kama ambavyo nchi zingine zinavyofanya.

Mwenyekiti Ngalula amesema kuwa katika miaka 21 ya TPSF serikali imeweza kuondoa vikwazo zaidi ya 40 hali ambayo imefanya sekta binafsi kuendelea na kutoa mchango kwa nchi pamoja wananchi.

Ngalula amesema sekta binafsi inaendelea katika kujiimarisha na kuongeza wanachama ambapo ni kutaka kuendelea kukua zaidi  kwa kutanua uwigo wa biashara.

Amesema wanamshukuru Rais Samia Hassan Suluhu kwa kufungua milango na mataifa mbalimbali.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 21wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF),uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Taasisi  ya Sekta Binafsi Tanzania(TPSF) Angelina Angalula akizungumza kuhusiana na mchango wa Sekta Binafsi katika Mkutano  Mkuu wa 21 wa Taasisi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uwekezaji Godfrey Mwambe akizungumza kuhusiana na Uwekezaji nchini kwa wafanyabiashara katika Mkutano Mkuu wa 21wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Viwanda na Biashara  akizungumza kuhusiana  wafanyabiashara katika Mkutano Mkuu wa 21wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) uliofanyika jijini Dar es Salaam. Uwekezaji nchini kwa wafanyabiashara katika Mkutano Mkuu wa 21wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa  Tamisemi Ummy Mwaimu  akizungumza kuhusiana na  Sekta Binafsi kuwekeza katika maeneo ya vijijini  nchini kwa wafanyabiashara katika Mkutano Mkuu wa 21wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya wanachama wa sekta binafsi  wakiwa katika Mkutano Mkuu wa 21 wa Taasisi ya  Sekta Binafsi Tanzania(TPSF)uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...